emblem

Chuo cha Diplomasia

Habari

Ziara ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki


Chuo cha Diplomasia(CFR) kimeagizwa  kufanya tafiti  mahsusi za kusaidia utatuzi wa changamoto mbalimbali kwenye jamii hususani za kistratejia na kiintelijensia na kusimamia kwa ukaribu utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa chuo hicho.
Rai hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) alipotembelea chuo hicho na kuzungumza na watumishi wake.