emblem

Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim

Habari

MAHAFALI YA 26 YA KITUO CHA UHUSIANO WA KIMATAIFA CHA DKT. SALIM AHMED SALIM.


SERIKALI YAKITAKA KITUO 

CHA UHUSIANO WA KIMATAIFA CHA DKT. SALIM 

KUTOA ELIMU BORA YA DIPLOMASIA, STRATEJIA 

 

Serikali imekitaka Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha 

Dkt. Salim Ahmed Salim kuhahikisha kinaendelea kutoa 

elimu bora ya Uhusiano wa Kimataifa, Diplomasia na 

Stadi za Stratejia. 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika 

Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb.) 

ambaye alimwakilisha Waziri wa Mambo ya Nje na 

Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January 

Makamba (Mb.) ametoa agizo hilo katika mahafali ya 26 

ya Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim 

Ahmed Salim na kuwatunuku vyeti wahitimu 1,008. 

Wahitimu hao wametunukiwa vyeti katika maeneo ya 

Uhusiano wa Kimataifa na Diplomasia, Diplomasia ya 

Uchumi, Usimamizi wa Amani na Migogoro na Utawala wa kimkakati

"Wizara inapenda kusisitiza umuhimu wa Kituo 

kuendelea kuelimisha Taifa kupitia mijadala na 

makongamano kwa lengo la kupanua uelewa wa 

masuala mbalimbali. Kituo kinapaswa pia kuendelea 

kusimamia na kutekeleza Majukumu ya Msingi ya 

kuanzishwa kwake ambayo yanajumuisha Taaluma, 

Utafiti na Ushauri Elekezi," alisema Balozi Mbarouk. 

Balozi Mbarouk aliongeza kuwa ni vyema Kituo 

kikaboresha progamu zake ili kukidhi mahitaji ya Wizara, 

Nchi na watanzania kwa ujumlawake,ambapo alishauri 

kuwa Kituo kiendelee kutoa elimu ya masuala 

mbalimbali yanayohusiana na Uhusiano wa Kimataifa, 

Diplomasia ya Uchumi na Stratejia kwa taasisi za 

Serikali na sekta binafsi ili kusaidia kukuza ujuzi wa 

wananchi wetu. 

"Naelekeza usimamie utekelezaji wa mabadiliko 

yanayoendelea kama ilivyopendekezwa na Kamati ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kutathmini utendaji kazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika 

Mashariki na taasisi zilizo chilli yake," Aliongeza Balozi 

Mbarouk.

Aidha ,Dkt,Jacobu nduye Kaimu mkurugenzi wa utawala na fedha katika kituo cha Dkt Salim Ahmed Salimu akimshukuru Mungu kwa kufanikisha tukio hilo la maafali, ameeleza kuhusu kituo hicho  kuandaa mpango mkakati wa utekelezaji katika Diplomasia ya uchumi. Ameeleza pia kuhusu   mafunzo mbalimbali yanayotolewa katika Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt.Salimu Ahmed Salimu ,ikiwa ni ya muda mrefu na  ya muda mfupi katika ngazi  ya Astashahada ya awali ya Uhusiano wa kimataifa na Diplomasia,Astashahada ya Uhusiano wa Kimataifa na Diplomasia,Stashahada ya Uhusiano wa Kimataifa na Diplomasia,Stashahada ya juu ya Uhusiano wa Kimataifa na Diplomasia,Shahada ya Uhusiano wa Kimataifa,Stashahada ya Uzamili ya mahusiano ya Kimataifa,Stashahada ya Uzamili katika Amani na Menejiment ya migogoro na Shahada ya Uzamili ya utawala wa kimkakati.

Kituo  kinatoa mafunzo ya lugha mbali mbali za kigeni ,ikiwemo  kireno ,kichina ,kiarabu,kihispania,kifaransa na kikorea .Pia chuo hicho kinatoa mafunzo  maalumu ya muda mfupi kwa wadau mbalimbali wakiwemo watumishi wa Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.alieleza Dkt. Jacob Nduye.