Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Kituo cha Uhusiano wa kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim
CEO

Ujumbe kutoka kwa Mkurugenzi

Katika mazingira ya kimataifa yanayobadilika kwa kasi, Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim kinatumika kama kitovu cha mafunzo ya kitaaluma, tafiti zenye mwelekeo wa kisera na majadiliano yenye tija. Katika kujibu mahitaji ya diplomasia mpya yenye masuala mtambuka na yaliyochangamana, Programu zetu zimebuniwa kukuza umahiri wa uchambuzi, uongozi wenye maadili, na ujuzi wa vitendo unaohitajika kukabiliana na changamoto mpya za kidiplomasia na maendeleo.

Kwa kuzingatia dira ya Taifa ya Maendeleo, Kituo kinatoa mchango katika kuandaa Viongozi wenye weledi na uwezo wa kuendeleza diplomasia ya uchumi, kuimarisha ushirikiano wa kimataifa, na kulinda maslahi ya taifa katika jitihada za kufikia maendeleo endelevu.

Kupitia ushirikiano wa kimkakati na kubadilishana maarifa, Kituo kinaendelea kuunga mkono ushirikiano wa kikanda na ushiriki wenye tija katika jukwaa la kimataifa. Tunaendelea kujizatiti katika kujenga jamii ya wataalamu wenye uwezo wa kuchangia  kikamilifu katika mwelekeo wa Tanzania kimataifa na hadhi yake duniani.

Tumejizatiti katika kuendeleza ubora wa hali ya juu katika nyanja za diplomasia, uhusiano wa kimataifa na uongozi wa kimkakati katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tukiongozwa na misingi ya Sera yetu ya Mambo ya Nje, tunaendelea kuimarisha uwezo wa taifa kushiriki kikamilifu na kwa ufanisi katika masuala ya kikanda na kimataifa.

Karibu uperuzi tovuti yetu, ambayo ninaimani itakuwa na manufaa kwako


Karibu!.

 

Dkt Felix Wandwe
Mkurugenzi

NEWS & UPDATES

News Image

KITUO CHA UHUSIANO WA KIMATAIFA CHA DKT. SALIM AHMED SALIM CHATOA WITO KWA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA...

News Image

MAFUNZO YA ITIFAKI NA UHUSIANO WA KIMKAKATI NA SERIKALI KATIKA KITUO CHA DKT. SALIM AHMED SALIM (CFR...

News Image

BALOZI WA CUBA NCHINI TANZANIA ATOA MHADHARA KATIKA KITUO CHA DKT. SALIM AHMED SALIM

News Image

KITUO CHA UHUSIANO WA KIMATAIFA CHA DKT. SALIM AHMED SALIM-CFR, CHAPOKEA UJUMBE KUTOKA CHUO CHA JES...

News Image

USAJILI WA WANAFUNZI WAPYA KWA MWAKA 2025/2026 KATIKA KITUO CHA UHUSIANO WA KIMATAIFA CHA DKT.SALIM...

News Image

INDIA KUTOA FURSA ZA UFADHILI WA MASOMO KWA WAHITIMU WA CFR

Dr. Salim Ahmed Salim Centre For Foreign Relations
Numbers 2025/26

Icon

1273

Higher Diploma Students

Icon

12

Programmes Offered

Icon

99

Employees

Icon

1560

Wanafunzi wa Diploma

Machapisho

Sheria
Sheria Ndogo za Wanafunzi
Mpango Mkakati
Fomu
Vipeperushi

ANNOUNCEMENTS

Usajili wa Wahitimu
Imechapishwa: 24 Apr 2026
New
WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MASOMO KITUO CHA UHUSIA...
Imechapishwa: 24 Apr 2026
New