Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Kituo cha Uhusiano wa kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim
Maadili

Kanuni Zetu Zinazoongoza

Maadili yetu ya msingi yanafafanua sisi ni nani, yanaongoza maamuzi yetu, na yanaunda dhamira yetu kwa ubora wa kitaaluma na ushirikiano wa kimataifa.

Uadilifu

Kuzingatia viwango vya juu vya uaminifu, maadili mema, uwajibikaji na uwazi katika utekelezaji wa majukumu yote ya Kituo.

Weledi

​​​​​​Kuzingatia viwango vinavyokubalika vya weledi na kuhakikisha ubora katika utoaji wa huduma zote za Kituo.

Ubora katika Huduma kwa Wateja

Kutoa huduma bora zinazokidhi na kuzidi matarajio ya wateja huku tukizingatia mahitaji yao yanayobadilika kila wakati.

Ushirikiano

Kukuza utamaduni wa kufanya kazi kwa pamoja, kuheshimiana na kuwajibika kwa pamoja katika kufanikisha malengo ya Kituo.

Ubunifu na Uvumbuzi

Kukuza mazingira yanayohamasisha kujifunza, ubunifu na uvumbuzi katika shughuli za kitaaluma na kiutawala ili kufanikisha malengo ya kimkakati ya Kituo.