Habari
WAFANYAKAZI WA KITUO CHA DKT.SALIM AHMED SALIM WAMEPATA MAFUNZO YA HUDUMA ZA PSSSF KWA NJIA YA MTANDAO
WAFANYAKAZI WA KITUO CHA DKT.SALIM AHMED SALIM WAMEPATA MAFUNZO YA HUDUMA ZA PSSSF KWA NJIA YA MTANDAO.
Watumishi wa Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt.Salim Ahmed Salimu leo wamepata mafunzo ya namna ya kupata huduma zinazotolewazo na mfuko wa hifadhi ya jamii wa utumishi wa umma (PSSSF) kwa njia ya mtandao.
Alipofungua mafunzo hayo Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Fedha wa kituo Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt Salim Ahmed Salim, Dkt.Jacob Nduye amesema "kutokana na changamoto mbalimbali walizokuwa wanazipitia watumishi wanapohitaji huduma zitolewazo na mfuko huo,hivyo mafunzo hayo yataleta tija kwa watumishi na kuondoa usumbufu walikuwa wakiupata kipindi walipokuwa wakihitaji huduma katika mfuko huo .
Kwa upande wa mtekelezaji wa Mafunzo hayo ndugu Thadeus Rweyamba amesema"mafunzo hayo yamekusudia kuondoa urasimu kwa kuboresha huduma zake katika kutoa huduma bora kwa njia ya mtandao badala ya mfumo uliokuwa unatumika kwa njia ya karatasi .
Ameongeza kwa kusema mfumo huo utawasaidia wanachama kupata huduma mbalimbali ikiwemo ufuatiriaji wa mafao na huduma nyingine zinazotokana na mfuko huo.
