Balozi wa Jamhuri ya Cuba nchini Tanzania, Mheshimiwa Yordenis Despaigne Vera, leo ametembelea Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim na kutoa Mhadhara kwa jumuiya ya Kituo ikijumuisha wafanyakazi, wahadhiri, na wanafunzi.
Mhadhara huo ulikuwa na mada isemayo: "Uhusiano wa Kihistoria Kati ya Tanzania na Cuba: Mtazamo wa Kisiasa, Kiuchumi na Kijamii nchini Cuba." Kupitia mada hiyo, Balozi Vera alieleza chimbuko la uhusiano imara wa kidiplomasia baina ya nchi hizo ulioasisiwa na viongozi wakuu wa mataifa haya, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Fidel Castro.
Aidha, ametoa taswira ya sasa ya hali ya kisiasa, kiuchumi, na kijamii nchini Cuba, pamoja na fursa mpya za ushirikiano katika sekta za afya, elimu, na maendeleo ya kijamii.Ujio wa Balozi wa Cuba katika Kituo unatajwa na uongozi wa Kituo kuwa ni fursa adhimu kwa wanafunzi, wahadhiri na jumuiya ya Kituo kujifunza kuhusu hali ilivyo nchini Cuba kutoka kwa mwakilishi wake.
Balozi Vera alitumia muhadhara huo kushukuru Serikali ya Tanzania kwa kuendelea na mshikamano na Cuba katika majukwaa mbalimbali ya kimataifa kupinga vikwazo dhidi yake, akisema hatua hiyo inaonesha undugu na mshikamano wa kihistoria uliopo kati ya mataifa hayo mawili.
Akifunga mhadhara huo, Kaimu Mkurugenzi wa Taaluma, Utafiti na Ushauri wa kituo hicho, Bw. Avit Chami, alimshukuru Balozi Vera kwa kuwasilisha mada hiyo na kuwapatia wanafunzi pamoja na wafanyakazi wa kituo taarifa na ufahamu mpana kuhusu hali halisi ya Cuba na mwelekeo wa mahusiano yake na Tanzania.Balozi wa Jamhuri ya Cuba nchini Tanzania,
Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim ( CFR), kimetoa wito...
Mafunzo ya muda mfupi kuhusu Itifaki za Mashirika na Uhusiano wa Serikali (Corpo...
Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim, kimepokea ujumbe kut...
Mapema Novemba 17, 2025 Wazazi na watoto wao wakiwa na nyuso zenye matumaini ya...
Balozi wa India nchini, Mheshimiwa Bishwadip Dey, amefanya ziara rasmi katika Ki...